DALILI ZA UCHUNGU
https://youtu.be/ddJSr8zDEro
Zifuatazo ni Dalili za Mwanzoni za Kujifungua au Dalili za Mwanzoni za Uchungu.
1. Maumivu ya Mgongo na Kiuno Wakati fulani.
Wajawazito wengi hupata Maumivu haya kutokana na Ongezeko la Homoni ya Relaxin ambayo hulegeza Nyonga kwa ajili ya kuhakikisha kuwa Mtoto anaweza kupita kwenye Nyonga, wakati Mwingine hii Homoni huweza kuathiri Jointi na Ligamenti za Mwili mzima na Mjamzito hupata Maumivu Jointi nyingine za Mwili wake.
2. Mtoto Kushuka (Lightening).
Kuanzia Wiki ya 32 Mara nyingi Mtoto hushuka kwenda kwenye Nyonga tayari kwa ajili ya Kuzaliwa na Kutoka Duniani.
3. Kukojoa Mara kwa Mara.
Baada ya Mtoto Kushuka Mjamzito huanza kupata Dalili za Kukojoa Mara kwa Mara, Ni kwa sababu Kibofu Cha Mkojo hugandamizwa na sehemu ya Mtoto ambayo iko Chini kwenye Nyonga ya Mjamzito na kubanwa kwa Kibofu Kati ya sehemu hiyo ya Mtoto na Mfupa wa Kinena.
4. Kuchoka Mara kwa Mara na Kukosa Usingizi.
Maumivu katika kipindi cha Mwishoni mwa Ujauzito na Kukojoa Mara kwa Mara hii hupelekea Mjamzito kukosa Usingizi wa kutosha hivyo Muda mwingi huwa na Uchovu wa Mara kwa Mara.
5. Uzito kutoongezeka.
Kwa kawaida Mjamzito huongezeka Uzito wa Wastani wa 1kg katika kila Mwezi mmoja katika Kipindi cha Ujauzito lakini inapofika Mwishoni mwa Ujauzito Uzito huwa hauongezeki na wakati mwingine inawezekana kabisa Uzito hupungua ndio maana ni vema inapofikisha Wiki 42 ujifungue na hutakiwi kuzidisha Wiki 43 za Ujauzito.
6. Kuharisha.
Baadhi ya Wajawazito hupata Dalili ya Kuharisha hii ni Kutokana na Ongezeko la Homoni za Prostaglandins ambazo hupelekea Mfuko wa Uzazi kujikunja na kuweza kutoa Mtoto Wakati wa Kujifungua lakini pia huweza kupelekea Ongezeko kubwa la mjongeo wa Utumbo Mdogo hivyo huweza kupelekea Dalili za Kuharisha kwa Mjamzito.
Hutofautiana kati ya Mjamzito moja na mwingine.
7. Maumivu ya Kubana na Kuachia.
Maumivu ya kubana na kuachia hutokea katika kipindi chote Cha Ujauzito, Lakini endapo Maumivu hayo hayana Mpangilio maalumu basi huwa ni Dalili za Mwanzoni za Kujfngua

Comments
Post a Comment